Ni sare ya nne mfululizo kwa klabu ya Yanga sc baada ya jana kutoka sare na timu ya Coastal union katika mchezo wa ligi kuu uliofanyika katika uwanja wa Mkwakwani jijini Tanga.
Awali Yanga ilitoka sare ya 1-1 na Mbeya city kisha dhidi ya Prisons Fc na ikasafiri kuifuata Polisi Tanzania napo ikatoka sare ya 1-1 na jana pia ikapata matokeo ya bila kufungana na wagosi wa kaya.
Yanga imeambulia pointi 4 kati ya 12 katika michezo minne na itahitaji kushinda mechi zake 16 zilizosalia huku ikiwaombea Simba sc wapoteze mechi 6 kati ya 14 walizobakisha ili wawe mabingwa.
🎯 Usipitwe!
Kuwa wa kwanza kupata habari za moto za michezo nchini Tanzania na duniani kwa ujumla, moja kwa moja kwenye barua pepe yako kutoka SportsLeo Bongo!
- ✅ Matokeo ya mechi
- ✅ Uchambuzi wa kina
- ✅ Habari za ndanii ya timu zako pendwa
✉️ Quality content, no spam. Unsubscribe anytime.
Mpaka sasa Simba ipo kileleni ikiwa na pointi 62 huku Yanga ikiwa nafasi ya nne na pointi 41 baada ya kucheza mechi za wikiendi hii japo ina michezo miwili mkononi.