Home Soka Zahera Matatani

Zahera Matatani

by Sports Leo
0 comments

Kufuatia kipigo cha mabao 2-1 dhidi ya Pyramids Fc kocha wa timu ya Yanga sc Mwinyi Zahera ameingia matatani baada ya mashabiki wa klabu hiyo kumtaka ajiuzuru baada ya kutopata matokeo waliyoyatarajia katika mchezo huo uliofanyika jijini Mwanza.

Zahera anashutimiwa na mashabiki kutokana na mbinu zake katika mchezp huo ambapo alijaza viungo wengi na kuacha mshambuliaji mmoja pekee ambaye alishindwa kufurukuta katika mchezo huo.

Mabao ya Pyramids yalipatikana kutokana na mbinu hiyo ya Zahera kutofungua uwanja huku baadae alipobadilisha mbinu kwa kuwaingiza Patrick Sibomana na Juma Balinya na kusababisha kupata bao dakika za mwishoni lililofungwa na Tshitshimbi.

banner

Mashabiki walimzomea na kumpiga chupa kocha huyo wakimshinikiza ajiuzuru huku wakiimba nyimbo za kumtaka aondoke.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited