Home Makala Yanga sc Yatua Mali

Yanga sc Yatua Mali

by Sports Leo
0 comments

Msafara wa wachezaji na viongozi wa klabu ya Yanga sc umefanikiwa kutua salama jijini Bamako nchini Mali kwa ajili ya mchezo wa raundi ya tatu ya michuano ya kombe la shirikisho dhidi ya Real Bamako ya nchini humo utakaofanyika siku ya Jumapili jioni.

Kikosi hicho kilivyotua nchini humo na moja kwa moja kuelekea hotelini ambapo masafara huo uliondoka Dar es salaam alfajiri ya Alhamis baada ya kumaliza kupata alama tatu dhidi ya Kmc katika mchezo wa ligi kuu nchini.

Yanga sc haikupata tabu baada ya kuingia nchini humo kutokana na uwepo wa wachezaji raia wa Mali katika kikosi hicho ambao ni Djigui Diarra na Mamadou Doumbia ambao nao ni maarufu nchini humo.

banner

Yanga sc watafuta alama tatu baada ya kuifunga Tp mazembe kwa mabao 3-1 katika mchezo wa kombe la shirikisho barani Afrika ambapo mpaka sasa wapo nafasi ya pili ya kundi hilo la D huku Real Bamako wakiwa nafasi ya mwisho ya msimamo wa kundi hilo.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited