Home Soka Manula Asaini Mitatu Simba

Manula Asaini Mitatu Simba

by Dennis Msotwa
0 comments

Kipa namba moja wa Timu ya Taifa ya Tanzania (Taifa Stars) Aishi Manula ameongeza mkataba mpya wa miaka mitatu na klabu yake ya sasa ya Simba Sports Club yenye makao makuu msimbazi jijini Dar es salaam.

Manula aliyetokea Azam Fc ambayo ilimkuza kisoka baada ya kutumikia kikosi cha timu pili cha timu hiyo(timu ya vijana) na baadaye kupandishwa kikosi cha wakubwa na kufanikiwa kumvua namba mkongwe Mwadini Ally na kisha kuondoka kwa wanalambalamba wa chamazi miaka miwili iliyopita na kujiunga na Simba sc.

Hivi sasa manula ni miongoni wa wachezaji wenye mafanikio kikosini hapo akifanikiwa kuwapa taji la ubingwa wa ligi kuu Tanzania bara kwa mara ya pili mfululizo huku akifanikiwa kuchukua tuzo ya kipa bora wa timu hiyo kwa mara ya pili mfululizo.,

banner

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited