Home Soka Ambokile Atua Tp Mazembe

Ambokile Atua Tp Mazembe

by Sports Leo
0 comments

Mshambuliaji wa Mbeya City Fc Eliud Ambokile amejiunga na wababe wa soka la Afrika kutoka Kongo Tp Mazembe kwa mkataba wa miaka mitatu akitokea Black Leopard ya Afrika ya Kusini alipokua anacheza kwa mkopo.

Inadaiwa klabu hiyo ambayo ni mabingwa mara tano wa klabu bingwa Afrika wamelipa takribani shilingi milioni 50 ili kupata saini ya mshambuliaji huyo mfupi mwenye nguvu na kasi anayetumia vizuri mguu wa kulia.

Ambokile amesajiliwa na Tp Mazembe ili kuziba nafasi ya mshambualiaji Ibrahim Ajibu ambaye walitaka kumsajili lakini walishindwana maslahi binafsi na mchezaji huyo huku taarifa zikidia tayari mchezaji huyo alikua na mkataba na Simba sc.

banner

Inatarajiwa Ambokile ataanza kuonekana na Mazembe katika michuano ya kombe la Kagame yatakayofanyika Kigali nchini Rwanda ambapo Mazembe watakua wageni waalikwa.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited