Home Makala Azam Fc Hali tete

Azam Fc Hali tete

by Sports Leo
0 comments

Klabu ya Azam Fc imezidi kujiwekea mazingira magumu ya kujinyakulia taji la ligi kuu nchini baada ya kulazimishwa suluhu na klabu ya Tabora United katika mchezo uliofanyika katika uwanja wa Ali Hassan Mwinyi mkoani Tabora.

Azam Fc iliyoanza bila mshambuliaji wake Prince Dube ilikua na wakati mgumu kupata nafasi ya kuipenya safu ya ulinzi wa Tabora United iliyokua chini ya beki kisiki Rajabu Zahir ambaye aliwadhibiti washambuliaji wa Azam Fc akianza na Abdul Sopu kisha Dube ambaye alingia kipindi cha pili.

Mpaka mpira unaisha Azam Fc haikupiga shuti lolote lililolenga lango licha ya kumiliki mpira kwa asilimia kubwa katika mchezo huo.

banner

Kutokana na sare hiyo sasa Azam Fc imekua katika nafasi ya pili ya msimamo ikiwa na alama 36 huku Yanga sc ikiwa kileleni mwa msimamo na alama 43 huku timu zote zikiwa zimecheza michezo 16 ya ligi kuu ya Nbc.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited