Home Makala Simba Sc Mambo Magumu Misri

Simba Sc Mambo Magumu Misri

by Sports Leo
0 comments

Klabu ya Simba Sc imepoteza mchezo wa kwanza wa hatua ya robo fainali ya michuano ya kombe la Shirikisho barani Afrika baada ya kukubali kipigo cha mabao 2-0 kutoka kwa Al Masry katika mchezo uliofanyika katika uwanja wa Suez Canal nchini Misri.

Simba sc ilijikuta ikikubali mabao mepesi licha ya kucheza mechi hiyo vizuri kwa dakika zote tisini ambapo walikua wanaongoza kwa kumiliki mpira na kutengeneza nafasi za kufunga.

banner

Simba sc iliyomkosa beki wake Che Malone Fondoh ilitanguliwa kufungwa kwa shuti kali la Abderahim Deughemom dakika ya 16 lililomshinda kipa Moussa Camara kutokana na mpira kudunda.

Bao hilo lilidumu mpaka kipindi cha pili ambapo pia simba sc walikosa nafasi kadhaa kupitia kwa Lionel Ateba na Kibu Dennis.

Kipindi cha pili Al Masry waliendelea kushambulia kwa kushtukiza huku wakiubana uwanja na kufanikiwa kuwadhibiti Simba sc ambao walikua wanacheza kwa maelewano na kushambulia kwa kasi.

Teknolojia ya mwamuzi wa njia ya video iliwafaidisha Al Masry baada ya mwamuzi kuwapa bao la pili ambalo awali ilidhaniwa kuwa ni mfungaji ameotea ambapo mpira uliopanguliwa na Moussa Camara ulimgonga Mshambuliaji wa Al Masry John Okoye na kuwapa wenyeji bao la pili.

Mpaka dakika 90 zinamalizika Simba sc walikubali kichapo hicho na sasa wana kazi kubwa ya kufanya April 9 2025 watakapovaana na timu hiyo katika mchezo wa marudiano.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited