Ni mwaka wa neema jangwani ndi unavyoweza kusema kwa sasa baada ya timu hiyo kupokea dili nono la udhamini kutoka kampuni ya GSM kupitia magodoro ya Gsm foam ambao wameingia mkataba wa mwaka mmoja kuidhamini klabu hiyo.
Haya yamekuja siku chache baada ya timu hiyo kupata udhamini mwingine kutoka kampuni ya gesi inayomilikiwa na bilionea Rostam Aziz kupitia bidhaa ya Taifa Gas ambao wanakaa mikononi mwa jezi za timu hiyo.
Udhamini huo wa Gsm unabaki kuwa siri kwa upande wa maslahi kama ilivyo mikataba mingine ambayo timu hiyo imeingia hivi karibuni.
🎯 Usipitwe!
Kuwa wa kwanza kupata habari za moto za michezo nchini Tanzania na duniani kwa ujumla, moja kwa moja kwenye barua pepe yako kutoka SportsLeo Bongo!
- ✅ Matokeo ya mechi
- ✅ Uchambuzi wa kina
- ✅ Habari za ndanii ya timu zako pendwa
✉️ Quality content, no spam. Unsubscribe anytime.
Hivi sasa Yanga ina udhamini wa makampuni kadhaa makubwa ikiwemo Sportpesa ambao ni wadhamini wakuu wanaokaa kifuani huku kampuni ya maji ya Watercom kupitia maji ya afya wakidhamini kama kinywaji kikuu cha kampuni hiyo wakati wa mechi na mazoezi na Taifa gas ambao hukaa mkononi huku Gsm foam watakaa mgongoni juu ya namba ya jezi.