Home Soka Gwambina Wairejesha Yanga Usiku

Gwambina Wairejesha Yanga Usiku

by Sports Leo
0 comments

Baada ya kulazimishwa matokeo ya suluhu dhidi ya Coastal Union jana, kikosi cha Yanga kilisafiri usiku kwa usiku kurejea jijini Dar es salaam kujiandaa na mchezo wa kombe la FA dhidi ya Gwambina FC

Mchezo huo utapigwa kweshokutwa Jumatano Februari 26 kwenye uwanja wa Taifa ambapo Yanga inatakiwa ishinde ili kuendelea na hatua inayofuatia.

Kutokana na mwenendo wa kusuasua kwenye ligi, Yanga italazimika ‘kukomaa’ na FA ili kuhakikisha inatwaa taji hilo kupata nafasi ya kushiriki michuano ya Shirikisho barani Afrika msimu ujao Kwani Matumiani ya kutwaa taji la ligi kuu tayari yametoweka.

banner

Baada ya kutoka suluhu hapo jana ili Yanga iwe bingwa wa ligi kuu inatakiwa ishinde mechi zake zote zilizosalia huku Simba ipoteze mechi sita kati ya 14 ilizobakiza.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited