Home Soka Makambo Anukia YANGA

Makambo Anukia YANGA

by Sports Leo
0 comments

Habari ya mjini ni kwamba yule straika anayefunga kwa kichwa na miguu yote Heritier Ebenezer Makambo anarudi Jangwani baada ya kuuzwa msimu uliopita katika klabu ya Horoya Fc ya nchini Guinnea.

Makambo aliyekuwa mfungaji bora katika kikosi cha Yanga msimu uliopita huku kwenye ligi akizidiwa na Meddie Kagere  wa Simba na Salim Aiyee aliyekua anaichezea Mwadui Fc.

Taarifa za ndani zinadai klabu hiyo kupitia kwa wadhamini wake kampuni ya Gsm tayari wameshakubaliana maslahi binafsi na mshambuliaji huyo na kilichobaki ni mazungumzo na klabu yake kuhusu kununua mkataba wake au kumchukua kwa mkopo.

banner

Kwa  mujibu wa ripoti ya kocha wa klabu hiyo Luc Eymael anahitaji mshambuliaji wa maana baada ya waliokuwepo wakiongozwa na David Molinga na Yikpe Gnamien kuchemka na wanatarajiwa kupewa mkono wa kwaheri.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited