Home Soka Ateba Aimaliza Pamba Jiji Fc

Ateba Aimaliza Pamba Jiji Fc

by Sports Leo
0 comments

Bao la penati dakika ya 23 la Lionel Ateba limeiwezesha klabu ya Simba Sc kuchukua alama tatu katika mchezo wa ligi kuu dhidi ya Klabu ya Pamba Jiji uliofanyika jioni ya leo katika uwanja wa Ccm Kirumba jijini Mwanza.

Ateba alifunga bao hilo baada ya kupokea pasi ya Awesu Awesu na beki wa Pamba Jiji Fc kumchezea faulo wakati akitazamana na kipa Yona Amos na ndipo mwamuzi alipoamuru pigo huru la mkwaju wa penati.

Mchezo huo uliotawaliwa na mambo mengi ya nje ya uwanja tangu Simba sc ilipowasili jijini humo ambapo hali hiyo imesababisha shauku kubwa kwa mashabiki na vyombo vya habari ikijumlisha pia vyombo vya dola.

banner

Kutokana na hayo ya nje ya uwanja,ndani ya uwanja Mchezo huo ulikua wa kasi huku kila upande ukijitahidi kupata ushindi.

Simba sc sasa baada ya kuchukua alama tatu muhimu imefanikiwa kufikisha alama 28 kileleni mwa msimamo huku kwa upande wa wenyeji hali ikizidi kuwa tete kwani wamesaliwa na alama 8 pekee wakiwa wa pili kutoka mkiani licha ya kucheza michezo 12 mpaka sasa.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited