Home Soka Coastal Union Yaendelea na Safisha Safisha

Coastal Union Yaendelea na Safisha Safisha

by Sports Leo
0 comments

Baada ya kuachana na Kipa wake Raia wa Congo Dr Ley Matampi sasa klabu hiyo imetangaza kuachana na beki wake Hernest Malonga pamoja na Deus Lucas baada ya kuvunja mkataba wake klabuni hapo.

Malonga mchezaji wa zamani wa klabu ya Ihefu Fc ambayo sasa ni Singida Black Stars anaondoka klabuni hapo kwa makubaliano na uongozi wa Klabu hiyo kuvunja mkataba huo.

Pia uongozi wa klabu hiyo chini ya kocha Juma Mwambusi umeendelea na kusafisha kikosi hicho ili kuruhusu kufanya sajili mpya zenye tija kikosini humo.

banner

Mpaka sasa katika msimamo wa ligi kuu ya Nbc nchini Coastal Union ina alama 16 katika nafasi ya tatu ya msimamo wa ligi kuu ikiwa imecheza michezo 13 tu.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited