Home Makala Corona Yamkosesha Amani Manara.

Corona Yamkosesha Amani Manara.

by Sports Leo
0 comments

Afisa  habari wa klabu ya Simba Sc, Haji Manara amefunguka kuwa anakosa amani kwani kila anapowaza janga la virusi vya Corona hajui litakwisha lini pia anafikiria kama itawezekana tena dunia kurudi katika hali yake ya kawaida na watu kuendelea na shughuli zao kama ilivyokuwa awali bila kuwa na hofu zaidi.

Manara aliweka sauti kwenye ukurasa wake wa instagram akisema kuwa, “hivi tutarudi na watu tukaaminiana bila ya kukwepana, watu wataingia misikitini, makanisani kufanya ibada bila hofu?”

“Walimwengu mimi nina hofu sana, siku ya tatu hii najiuliza hili swali, hamuoni kama kuna jambo Mwenyezi Mungu anataka kutufundisha kitu kupita kwa haya maradhi aliyotuletea?sayansi itakataa ila mimi naamini ipo sababu ya Mungu katika jambo hili” alisema Manara.

banner

 

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited