Home Makala Feisal,Aucho Kuivaa Namungo Fc

Feisal,Aucho Kuivaa Namungo Fc

by Sports Leo
0 comments

Kikosi kamili cha klabu ya Yanga sc sasa kimerejea baada ya kocha msaidizi Cedrick Kaze kutangaza kwamba mastaa Khalid Aucho na Feisal Salum wanarejea kuivaa Namungo katika mchezo wa ligi kuu nchini utakaofanyika kesho katika uwanja wa Benjamin Mkapa jijini Dar es salaam.

Mastaa hao wanarejea baada ya kuwa na majeraha walipojitonesha wakiwa katika majukumu ya timu za Taifa na kusababisha kukosekana uwanjani kwa kipindi cha wiki kadhaa huku wakikosa michezo muhimu kama dhidi ya Azam Fc na Geita Gold ambapo Yanga sc iliteseka kupata ushindi.

Kaze ambaye ni kocha msaidizi wa klabu hiyo amebainisha wakati akizungumza na waandishi wa habari kwamba Aucho na Feisal wanaungana na Chico Ushindi na Farid Mussa kuongeza nguvu katika kikosi hicho huku akijinasibu kuwa watapata alama tatu dhidi ya Namungo ambayo haijafungwa na Yanga sc tangu ipande ligi kuu nchini.

banner

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited