Home Makala JKT Washindwa Mziki Wa Simba

JKT Washindwa Mziki Wa Simba

by Sports Leo
0 comments

Simba Sc imewapa kichapo cha mabao 4-0 JKT Tanzania katika mchezo wa raundi ya tano ya ligi kuu bara uliochezwa jana uwanja wa Jamuhuri mkoani Dodoma majira ya Saa 8:00mchana.

Meddie Kagere alipachika mabao mawili dakika ya 3′ na 41 huku Chris Mugalu naye hakuwa nyuma katika kipindi cha kwanza cha mchezo ambapo alicheka na nyavu dakika ya 6.

Bao lililokosha mashabiki wa Simba Sc na wakainuka wote uwanjani ni lile ambao lilipachikwa dakika ya 54 na Luis Miquissone ambapo lilidumu hadi dakika 90 za mchezo na kuwafanya wekundu hao kuondoka na alama tatu muhimu.

banner

Aishi Manula alikuwa na jitihada kubwa sana za kulinda lango la Simba Sc licha ya Mashambulizi kuwa mengi hakuruhusu bao lolote.

Katika msimamo wa ligi kuu Simba ipo nafasi ya 2 ikiwa imejikusanyia pointi 13 katika raundi ya 5 ya ligi kuu huku vinara wakiwa Azam Fc wenye pointi 15.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited