Home Makala Job,Feitoto Warejea Yanga sc

Job,Feitoto Warejea Yanga sc

by Sports Leo
0 comments

Mastaa wa klabu ya Yanga sc Dickson Job na Feisal Salum wamerejea uwanjani baada ya kumaliza adhabu zao za makosa ya utovu wa nidhamu ambazo ziliwafanya wakose michezo ya ligi kuu hasa ule dhidi ya Kagera Sugar siku ya Jumapili.

Feisal alikosa mchezo huo akikabiliwa na adhabu baada ya kuwa na kadi tatu za njano huku ya mwisho akiipata dhidi ya Mtibwa Sugar baada ya kufunga goli kwa kutumia mkono na mwamuzi kuamua kumzawadia kadi hiyo iliyomfanya akakosa mchezo dhidi ya Kagera Sugar ili kutumikia adhabu kwa mujibu wa kanuni.

Kwa upande wa Dickson Job alikosa jumla michezo mitatu kutokana na kufungiwa na bodi ya ligi kwa kosa la kumkanyaga Richarlison Ng’ondya wa Mbeya City katika  mchezo wa ligi kuu zilipokutana timu hizo mchezo ambao ulimalizika kwa suluhu.

banner

Jumla Job alizikosa mechi dhidi ya Biashara United,Mtibwa Sugar na Kagera Sugar huku klabu yake ikiibuka na ushindi katika michezo yote hiyo huku nafasi yake ikizibwa vyema na Yannick Bangala ambaye mara nyingi huchezeshwa eneo la kiungo.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited