Kiungo anayekipiga ndani yaklabu ya Yanga,Feysal Salum’Feitoto’ ambaye pia ni miongoni mwa viungo anayemkubali Clatous Chama wa Simba Sc ameonesha nia ya kuibukia huko kwa masharti.
Fei Toto kwa sasa yupo zake Visiwani Zanzibar baada ya ligi kusimamishwa kutokana na janga la Virusi vya Corona ila amesema kuwa anaweza kucheza ndani ya klabu ya Simba iwapo viongozi wake watamruhusu kufanya hivyo kwani bado ana mkataba mrefu na Yanga lakini hana shida iwapo itatokea klabu ya Simba ama nyingine zikahitaji saini yake.
“Mimi ni mchezaji wa Yanga viongozi wananipenda nami nawapenda pia ikitokea klabu inahitaji saini yangu utaratibu ufuatwe sina hiyana nitasaini bila tatizo,” alisema Feitoto
🎯 Usipitwe!
Kuwa wa kwanza kupata habari za moto za michezo nchini Tanzania na duniani kwa ujumla, moja kwa moja kwenye barua pepe yako kutoka SportsLeo Bongo!
- ✅ Matokeo ya mechi
- ✅ Uchambuzi wa kina
- ✅ Habari za ndanii ya timu zako pendwa
✉️ Quality content, no spam. Unsubscribe anytime.