Home Makala Kiungo Huyu Akubali Kutua Simba

Kiungo Huyu Akubali Kutua Simba

by Sports Leo
0 comments

Kiungo anayekipiga ndani yaklabu ya Yanga,Feysal Salum’Feitoto’ ambaye pia ni miongoni mwa viungo anayemkubali Clatous Chama wa Simba Sc ameonesha nia ya kuibukia huko kwa masharti.

Fei Toto kwa sasa yupo zake Visiwani Zanzibar  baada ya ligi kusimamishwa kutokana na janga la Virusi vya Corona ila amesema kuwa anaweza kucheza ndani ya klabu ya Simba iwapo viongozi wake watamruhusu kufanya hivyo kwani bado ana mkataba mrefu na Yanga lakini hana shida iwapo itatokea klabu ya Simba ama nyingine zikahitaji saini yake.

“Mimi ni mchezaji wa Yanga viongozi wananipenda nami nawapenda pia ikitokea klabu inahitaji saini yangu utaratibu ufuatwe sina hiyana nitasaini bila tatizo,” alisema Feitoto

banner

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited