Home Makala Kocha Tabora United Atua Dodoma Jiji Fc

Kocha Tabora United Atua Dodoma Jiji Fc

Aanza Usajili wa Mastaa Wapya

by Dennis Msotwa
0 comments

Aliyewahi kuwa Kocha wa Tabora United Fc  Anicet Kiazmak ametua katika timu ya Dodoma Jiji Fc ili kuinoa timu hiyo kwa ajili ya msimu ujao wa ligi kuu na michuano ya kombe la Shirikisho la Crdb nchini.

Uongozi wa Dodoma umeshafanya maamuzi ya kuachana na Kocha Mecky Maxime aliyekuwa na mkataba wa mwaka mmoja ili kupisha usajili ya Kiazmak ambaye aliifanya Tabora United kuwa timu tishio nchini.

Mpaka sasa Dodoma Jiji Fc na Kocha Anicet Kiazmak raia wa DR. CCongo wameshakubaliana kila kitu na kilichobaki ni kocha huyo kusaini mkataba na kuanza kazi moja kwa moja.

banner

Tayari kocha huyo ameshaanza kupendekeza majina ya wachezaji anaotaka kufanya nao kazi klabuni hapo na tayari klabu hiyo imesajili kiungo mkabaji raia wa Congo Drc Nelson Munganga kuja kuungana na kocha huyo.

Mbali na Munganga aliyekua nae Tabora United pia kuna mastaa kadhaa watatua klabuni hapo ikiwa ni matakwa ya kocha huyo kuisuka timu hiyo iwe ya ushindani mkubwa.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited