Home Makala Ligi Raundi Ya Sita Inaanza Hivi

Ligi Raundi Ya Sita Inaanza Hivi

by Dennis Msotwa
0 comments

Ligi kuu Tanzania Bara raundi ya sita inaendelea leo Octoba 14,ambapo timu nane zitavaana katika viwanja vinne tofauti kwaajili ya kusaka pointi tatu muhimu.

Raundi ya tano ilimalizika na kuwaacha Azam Fc wakiwa ni vinara kwa pointi 15 huku Simba Sc wakishika namba 2 na pointi 13 sawa na Yanga sc ambao wameshika nafasi ya tatu kwa mpishano wa mabao.

Leo katika raundi ya sita,Biashara United itawakaribisha Ihefu Fc uwanja wa Karume majira ya saa 10:00 jioni huku JKT Tanzania ikivaana na Ruvu Shooting saa 8:00 mchana katika uwanja wa Jamhuri jijini Dodoma.

banner

KMC ambao ni vijana wa Kinondoni itawakaribisha Coastal Union uwanja wa Uhuru saa 10:00 jioni huku Namungo Fc ikipambana dhidi ya Kagera Sugar uwanja wa Majaliwa majira ya saa 10:00 jioni.a

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited