Kuelekea mchezo wa ngao ya jamii baina ya Yanga sc na Simba sc utakaofanyika kesho katika uwanja wa Benjamin Mkapa jijini Dar es salaam makocha wa timu zote mbili Zoran Maki na Mohamed Nabi wamefunguka kuhusu mchezo huo ambao utakua ndio mchezo wa kufungua pazia la ligi kuu nchini.
Katika mkutano na waandishi wa Habari uliofanyika hivi punde katika makao makuu ya shirikisho la soka nchini (Tff) yaliyopo Karume makocha hao pamoja na manahodha John Boko na Bakari Mwamnyeto walipata wasaa wa kuzungumza machache.