Home Makala Mkude Kuikosa Berkane

Mkude Kuikosa Berkane

by Sports Leo
0 comments

Kiungo wa klabu ya Simba sc Jonas Mkude anatarajiwa kuikosa mechi dhidi ya Rs Berkane ya nchini Morroco katika mchezo wa tatu wa timu hiyo utakaofanyika leo usiku nchini Morroco ikiwa ni mchezo wa tatu wa klabu hiyo katika kundi D.

Hii ni mechi ya pili mfululizo kwa mkude kuikosa kutokana na kusumbuliwa na majeraha akiwa tayari amezikosa timu za Us Gendamirie katika sare ya moja moja ugenini na sasa atalazimika kuikosa Berkane.

Simba sc tayari ipo nchini Morroco ikitetea nafasi yake ya uongozi wa kundi D baada ya kuichapa Asec Mimosa na kutoa sare ugenini na Gendamarie na kushika uongozi wa kundi na sasa wana kibarua cha kuhakikisha wanapata alama tatu ugenini.

banner

Kutokana na kutokuwepo kwa mkude Simba sc inaweza kuwatumia Erasto Nyoni,Mzamiru Yassin ama Thadeo Lwanga ambaye amerejea kutoka majeraha kucheza sambaba na Saido Kanoute katika eneo la kiungo wa ulinzi.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited