Home Soka Morocco Atema Watatu Zanzibar Heroes

Morocco Atema Watatu Zanzibar Heroes

by Sports Leo
0 comments

Kocha wa timu ya Taifa ya Zanzibar Hemed Morocco amewatema mastaa watatu katika kikosi cha timu hiyo kilichoingia kambini Disemba 24 kujiandaa na michuano ya Mapinduzi Yanayotarajiwa kufanyika Visiwani humo kuanzia Januari 3 mwaka 2025.

Awali Morocco aliwaita zaidi ya wachezaji 20 katika kambi ya timu hiyo ambapo aliwataka kuripoti kambini Disemba 24 lakini mastaa Abdalah Said Lanso wa Kmc na Ibrahim Mkoko wa Namungo walichelewa kuripoti kambini bila taarifa maalumu hali iliyosababisha kutemwa katika kikosi hicho.

Mastaa hao wamechelewa kuripoti wakati tayari klabu zao zilishawapa ruhusa ndani ya muda muafaka.

banner

Baada ya wachezaji hao kutemwa kocha Morocco alimuita mchezaji Ali Said Mabata kutoka timu ya uhamiaji Fc kuchukua nafasi hiyo.

Ikiwa hilo halijasahaulika kwa wadau wa soka Visiwani humo,Kocha huyo kwa mara nyingine amemuondoka kikosini mchezaji Abdulaaziz Makame Bui wa Klabu ya Geita Gold Fc kutokana na kuchelewa kambini ambapo nafasi yake imechukuliwa na Abubakar Nizar wa klabu ya Azam Fc chini ya miaka 20 pamoja na Abdulnasir Abdalah Casemiro wa timu ya mlandege Fc.

Zanzibar Heroes imejizatiti kufanya vizuri msimu huu katika michuano ya kombe la mapinduzi ambalo linashirikisha timu za Taifa msimu huu na sio klabu kama ilivyozoeleka.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited