Home Makala Morrison Si Yanga Tena

Morrison Si Yanga Tena

by Sports Leo
0 comments

Mchezaji namba 28 aliyetambulishwa na Yanga Sc siku ya wananchi Agosti,31 Benard Morrison sio tena mchezaji wa klabu ya Yanga baada ya shirikisho la soka Tanzania (TFF) kumtambulisha rasmi kama mchezaji wa Simba Sc.

TFF imetoa uamuzi huo kwa kusimamia maamuzi ya kamati ya Sheria waliyompa Benard Morrison kuchagua timu anayohitaji kuitumikia na yeye akapendekeza Simba Sc kwani mahakama ilimtambulisha Mghana huyo kama mchezaji huru.

Katika usajili mpya wa TFF kwa msimu ujao wa ligi kuu bara jina la Morrison limetokezea Simba Sc hivyo inaonyesha ni mshambuliaji huyo ni mali rasmi ya wanamsimbazi na si wanajangwani.

banner

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited