Home Makala Mshery Kufanyiwa Upasuaji

Mshery Kufanyiwa Upasuaji

by Sports Leo
0 comments

Klabu ya Yanga sc imeamua kumpeleka nchini Morroco golikipa wake namba mbili AbouTwalib Mshery ambaye anasumbuliwa na goti ili apone haraka ambapo atafanyiwa upasuaji na wataalamu wabobezi wa masuala ya viungo.

Maamuzi hayo yamefikiwa kutokana na umuhimu wa kipa huyo wakati klabu hiyo ikielekea katika michuano ya kimataifa ambapo mpaka sasa inao makipa wengine watatu wakiongzowa na Djigui Diarra,Metacha Mnata ambaye yupo kwa mkopo wa miezi sita na Erick Johora.

Wataalamu hao ambao watamfanyia matibabu kipa huyo ni wale ambao walimtibu Kibwana Shomari na Yacouba Songne ambao nao walikua wakisumbuliwa na magoti.

banner

Mshery tangu asajiliwe Yanga sc amefanikiwa kuwa mbadala wa kudumu wa Djigui Diarra ambaye hata anapokosekana kinda huyo hufanya kazi nzuri inayowavutia mashabiki wa soka nchini.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited