Home Makala Mwamnyeto Ajifunga Yanga sc

Mwamnyeto Ajifunga Yanga sc

by Sports Leo
0 comments

Beki tegemeo wa klabu ya Yanga sc na Taifa Stars Bakari Mwamnyeto amesaini mkataba wa miaka miwili kusalia klabuni hapo baada ya ule wa awali kumalizika msimu huu.

Taarifa kutoka ndani ya Yanga sc zinasema kwamba beki huyo amesaini mkataba huo wenye thamani ya kiasi cha shilingi milioni 200 za kitanzania na kuzima tetesi za kuondoka klabuni hapo hasa alipokua akihusishwa na klabu ya Simba sc.

Yanga sc ilimsajili Mwamnyeto misimu miwili iliyopita akitokea Coastal Union ambapo amefanikiwa kuonyesha kiwango bora kabisa na kupewa unahodha wa klabu hiyo mbele ya mastaa kama Fiston Mayele na Yannick Bangala Litombo.

banner

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited