Home Makala Nabi Afunguka Kuwatimua Saido,Ambundo Kambini

Nabi Afunguka Kuwatimua Saido,Ambundo Kambini

by Dennis Msotwa
0 comments

 Kocha Mkuu wa klabu ya Yanga sc Nasredine Nabi amefunguka kuhusu sakata la kuwatimua kambini mastaa wake Saido Ntibazonkiza na Dickson Ambundo huku akijitetea kuwa alichukua uamuzi huo kwa manufaa ya timu kuelekea mchezo wa dhidi ya Simba sc.

Nabi alisema kuwatimua wachezaji hao hakuna suala lingine zaidi ya nidhamu bila kujali kama unahitaji matokeo ama ala pia akisisitiza kuwa hakuna timu inayomtegemea mchezaji mmoja.

“Hakuna timu inayomtegemea mchezaji mmoja hata iwe mchangani, kwenye klabu kubwa na inayojiheshimu kuna utaratibu ambao kila mtu anaujua na kama haufuatwi ni tatizo kwahiyo huwezi kuacha kufuata utaratibu kwa sababu unatafuta matokeo”. amesema Nabi.

banner

Ameongeza, “Ni kweli hicho kitu kimetokea lakini watu wanapaswa kujua wachezaji hawa hawakuwahi kuwa na tatizo hili la kinidhamu lakini kwa kuzingatia umuhimu wa mchezo na kuhitaji kudumisha utulivu kwenye timu tumelazimika kufanya hivyo, ni wachezaji wenye nidhamu siku zote wamekuwa na nidhamu na kuisaidia timu na wataendelea kuisaidia”.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited