Home Makala Serikali Yajiweka Pembeni Sakata la Derby

Serikali Yajiweka Pembeni Sakata la Derby

by Sports Leo
0 comments

Serikali kupitia kwa Naibu Waziri wa Habari,Utamaduni, Sanaa na Michezo Hamis Mwinjuma imesema kuwa haiwezi kuingilia mgogoro unaoendelea kuhusu mechi ya Darby kati ya Simba na Yanga kutokana na kuwepo mamlaka inayosimamia soka nchini ambayo ni Shirikisho la soka (TFF)

Mwinjuma amesema hayo bungeni jijini Dodoma mapema hii leo  wakati akijibu swali la nyongeza la mbunge wa Jimbo la makete Mh.Festo Sanga aliyetaka kujua hatima ya mvutano wa timu mbili za Simba sc  na Yanga sc  pamoja na TFF.

banner

“Shughuli za mpira wa mguu una mamlaka zake za kimataifa na za kitaifa na tumekuwa tukisisitizwa mara kwa mara serikali kutoingilia moja kwa moja  uendeshaji wa shughuli hizo ili kuepuka kuja kufungiwa nna Shirikisho la Soka Duniani (FIFA) kwa nyakati hizi hata kitakwimu nchi yetu inafanya vizuri katika uendeshaji wa shughuli za mpira wa mguu”,Alisema Mh.Hamis Mwinjuma Naibu Waziri wa Habari,Utamaduni, Sanaa na Michezo mbele ya wabunge bungeni humo.

“Kuhusu mchezo anaousema serikali inafuatilia kwa karibu jinsi ambavyo mgogoro huu unaendelea kutatuliwa lakini huku tukijaribu kwa kiwango kikubwa kutoingilia moja kwa moja maamuzi ya TFF na Bodi ya ligi” alimalizia kusema na kuamsha makofi kwa baadhi ya wabunge.

Mpaka sasa hali ya soka nchini imekua na sintofahamu kufuatia mgogoro huo ulioanza tangu machi 8 2025 baada ya klabu ya Simba Sc kugomea mchezo baina yake na Yanga sc baada ya siku moja kabla kuzuiwa kufanya mazoezi katika uwanja wa mechi kwa mujibu wa kanuni.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited