Home Makala Simba sc Yafungwa Guinnea

Simba sc Yafungwa Guinnea

by Sports Leo
0 comments

Klabu ya Simba sc imeshindwa kuibuka na ushindi katika mchezo wa kwanza wa ligi ya mabingwa barani Afrika ikikubali kichapo cha bao 1-0 kutoka kwa Horaya katika mchezo uliofanyika nchini Guinnea.

Simba sc ilifungwa bao hilo kwa kichwa dakika ya 18 ya mchezo likifungwa na Pape Ndiaye na lilidumu mpaka dakika tisini za mchezo licha ya jitihada za Simba sc kusawazisha bao hilo kushindikana huku John Bocco akikosa takribani nafasi mbili zawazi na Horoya wakikosa penati iliyookolewa na Kipa wa Simba sc Aishi Manula.

Pamoja na Simba sc kuanza mchezo na viungo watatu wa ukabaji Mzamiru Yassin,Sadio Kanoute na Sawadogo walishindwa kutawala mchezo ambapo walichangamka baada ya kuingia kwa Bocco,Kibe Dennis na Habib Kyombo lakini mabadiliko hayo hayakubadili matokeo ya mchezo huo.

banner

Simba sc sasa inawasubiri Raja Casablanca katika mchezo wa pili utakaofanyika wikiendi ijayo katika uwanja wa Benjamini Mkapa jijini Dar es salaam.

 

 

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited