Home Makala Simba Sc Yafuzu Nusu Fainali Crdb

Simba Sc Yafuzu Nusu Fainali Crdb

by Sports Leo
0 comments

Ushindi wa mabao 2-1 ilioupata klabu ya Simba Sc dhidi ya Klabu ya Bigman Fc umeivusha moja kwa moja katika hatua ya nusu fainali ya kombe la Shirikisho la Crdb nchini.

Simba sc ilipata Ushindi huo jioni ya leo katika mchezo uliofanyika katika uwanja wa Kmc Complex uliopo Mwenge jijini Dar es Salaam na kuvuka hatua hiyo.

Kocha Fadlu Davis alimuanzisha kipa Hussein Abel huku mabeki wa kati wakicheza Duchu sambamba na Hussein Kazi na safu ya ushambuliaji iliongozwa na Lionel Ateba.

banner

Joshua Mutale leo aliifungia Simba sc bao la kwanza dakika ya 15 ya mchezo akiunganisha pasi ya Valentino Nouma aliyecheza upande wa kushoto na kuipatia Simba sc bao la uongozi.

Dakika ya 30 ya mchezo huo Lionel Ateba aliifungia Simba sc bao la pili kwa penati baada ya beki wa Bigman Fc kumuangusha Ellie Mpanzu katika eneo la hatari.

Kipindi cha kwanza Joseph Henock aliipa bao la kifutia machozi klabu yake ya Bigman akifunga bao kwa shuti kali lililomshinda kipa Hussein Abel dakika ya 44 ya mchezo.

Mpaka dakika 90 zinakamilika Simba sc ilikata tiketi ya kufuzu hatua inayofuatia huku Bigman Fc ikiaga mashindano moja kwa moja.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited