Home Makala Simba sc Yaleta Mtaalamu wa Usajili

Simba sc Yaleta Mtaalamu wa Usajili

by Sports Leo
0 comments

Klabu ya Simba sc imeazimia kuajiri mkurugenzi wa ufundi kwa ajili ya kusimamia mambo yote ya kiufundi ikiwemo usajili wa mastaa mbalimbali watakaoitumikia klabu hiyo tofauti na sasa ambapo usajili unafanywa na kamati maalumu ya usajili.

Simba sc imefikia kufanya hilo baada ya kusajili mastaa wengi ambao wameshindwa kuisaidia timu hiyo moja kwa moja hasa katika misimu hii miwili ya 2020/2021 na 2021/2022 ambapo klabu hiyo imemaliza bila kupata kombe lolote huku mafanikio pekee yakiwa ni kufuzu hatua ya robo fainali ya michuano ya Caf.

Simba sc ilimsajili Ismaël Sawadogo kipindi cha dirisha dogo lakini mchezaji huyo ameshindwa kuonyesha kiwango hali iliyopelekea mashabiki na wadau wa soka nchini kuzua mjadala kuhusu vigezo vilivyotumika kumsajili mchezaji huyo.

banner

Inasemekana kuwa bosi wa klabu hiyo Mohamed Dewji ameridhia suala la kuajiriwa kwa mkurugenzi wa ufundi huyo huku kocha Roberto Oliveira ameruhusiwa kuamua nani aajiriwe katika nafasi hiyo.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited