Home Makala Singida Black Stars Washangaa Miloud Kutua Yanga Sc

Singida Black Stars Washangaa Miloud Kutua Yanga Sc

by Sports Leo
0 comments

Klabu ya Singida Black Stars imetangaza kushtushwa na taarifa ya kocha wake Hamdi Miloud kujiunga na klabu ya Yanga sc kutokana na kuwa na mkataba naye.

Jana usiku klabu ya Yanga sc ilitangaza kuondoka kwa kocha Sead Ramovic na msaidizi wake huku ikimtangaza Miloud kuwa kocha mpya wa klabu hiyo.

banner

Taarifa iliyotolewa na idara ya habari ya klabu ya Singida Black Stars imesema kuwa uongozi wa klabu hiyo utachukua hatua ambapo kwa sasa imewaomba mashabiki kuwa watulivu wakati uongozi ukishughulikia suala hilo.

Miloud anaondoka klabuni hapo ambapo amezifundisha klabu ya Singida Black Stars kwa takribani mwezi mmoja pekee akisimama kama kocha mkuu katika michezo miwili ya kirafiki dhidi ya Tma na Mbuni Fc ambazo zote aliibuka na ushindi.

 

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited