Home Makala Stars Kuingia Kambini J’pili

Stars Kuingia Kambini J’pili

by Sports Leo
0 comments

Timu ya soka ya Tanzania(Taifa stars) inatarajiwa kuingia kambini siku ya jumapili ili kujiandaa na mchezo wa kufuzu fainali za mataifa ya Afrika kwa wachezaji wa ndani(Chan) zitakazofanyika nchini Cameroon Mwaka 2020.

Mchezo huo dhidi ya Sudan utafanyika mjini Kigali nchini Rwanda baada ya wenyeji kuchagua nchi hiyo baada ya Caf kuzuia mchezo huo kufanyika nchini Sudan kusini kwa sababu za kiusalama kisha marudiano yatafanyika nchini baada ya wiki mbili toka mchezo wa kwanza.

Tanzania imepata nafasi hiyo ya kucheza mechi hiyo baada ya kufanikiwa kuitoa Kenya kwa mikwaju ya penati mjini Nairobi baada ya awali kutoka sare ya 0-0 jijini Dar es salaam.

banner

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited