Home Makala Stars Yalala 2-0 kwa Algeria

Stars Yalala 2-0 kwa Algeria

by Sports Leo
0 comments

Timu ya Taifa ya Tanzania (Taifa stars) imekubali kichapo cha mabao 2-0 kutoka kwa Algeria katika mchezo wa kuwania kufuzu michuano ya Afcon mwakani zitakazofanyika nchini Ivory Coast.

Katika mchezo huo wa pili kwa Stars katika kundi baada ya awali kupata sare ya 1-1 ugenini dhidi ya Niger,iliwalazimu Algeria kusubiri mpaka mwishoni mwa kipindi cha kwanza kupata bao la uongozi kupitia kwa Amir Selmane aliyefunga kwa kichwa kutokana na uzembe wa mabeki wa Stars kuokoa mpira wa faulo.

Kocha Kim Poulsen Kipindi cha pili aliweza kufanya mabadiliko kwa  kuwaingiza Kibu Dennis, George Mpole, Kelvin John na Salum Abubakar huku waliotoka ikiwa ni Feisal Salum,Simon Msuva,Nickosn Kibabage na Novatus Dismas ambao walibadili mchezp lakini hawakuwa na madhara kwa wageni kwani mashambulizi mengi yalidhibitiwa kabla ya kufika kwa kipa.

banner

Wakati Stars ikisaka bao la kusawazisha Algeria walipata mpira na kufanya shambulio la kushtukiza na kufanikiwa kupata bao la pili kupitia kwa Mohamed El Amine dakika ya 89′ na kufanya mchezo kumalizika kwa Stars kupoteza alama tatu muhimu.

Kutokana na matokeo hayo sasa Algeria anaongoza kundi F akiwa na alama 6 huku Niger akiwa na alama 2 na Tanzania na Uganda zikiwa na alama 1 kila mmoja.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited