Home Makala Yacouba Kukiwasha Mapinduzi Cup

Yacouba Kukiwasha Mapinduzi Cup

by Sports Leo
0 comments

Mshambuliaji wa Yanga Yacouba songne ataanza kuwatumikia Wananchi kwenye mashindano ya mapinduzi cup visiwani Zanzibar yanayotarajiwa kuanza mwanzoni mwa mwezi January mwakani visiwani Zanzibar.

Kocha mkuu wa Yanga Professor Mohamed Nasreddine Nabi amepanga kumpa nafasi ya kutosha Yacouba songne kwenye mashindano ya hayo kabla hajamrudisha rasmi kwenye kikosi ambacho kinacheza mashindano yote ya ndani na nje huku ikitarajiwa kwamba anaweza kuchukua nafasi ya staa mmoja wa kigeni kikosini humo.

Pia inasemekana kwamba Professor Mohamed Nasreddine Nabi amepanga kuyatumia mashindano ya kombe la mapinduzi Kama sehemu ya kuiandaa timu kabla ya kuanza michezo ya kimataifa kwenye ngazi ya makundi ambapo Yanga sc wamepangwa katika kundi D na Timu za Tp Mazembe,Real Bamako na El Monastry ya nchini Hispania.

banner

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited