Home Makala Yanga Sc Kamili Kuivaa Prisons Fc

Yanga Sc Kamili Kuivaa Prisons Fc

by Sports Leo
0 comments

Klabu ya Yanga sc ipo tayari kwa mchezo wa ligi kuu ya Nbc nchini dhidi ya Tanzania Prisons utakaofanyika katika uwanja wa Kumbukumbu ya Sokoine jijini Mbeya jioni ya saa 10.

Tayari kikosi kamili cha klabu hiyo kipo jijini humo kwa ajili ya mchezo huo na leo kocha Miloud Hamdi amethibitisha utayari wa kikosi chake wakati akizungumza na waandishi wa habari jijini humo.

“Maandalizi yetu yapo vizuri sana, tuna fainali nne za kucheza. Tupo tayari kuukabili mchezo wa kesho kikamilifu. Kila mchezaji anajua kitu gani cha kufanya kesho. Kikosi chetu kipo kamili hakuna majeruhi wapya. Hatuna presha yoyote na hatuna sababu ya kuwa na presha”alisema kocha huyo.

banner

Mchezo huo wa ligi kuu ya NBC kati ya Tanzania Prisons dhidi ya Yanga SC utachezeshwa na mwamuzi Abdallah Mwinyimkuu kutoka mkoani Singida, atasaidiwa na Makame Mdogo wa Shinyanga na Wema Kalinga wa Dodoma Dodoma.

 

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited