Home Soka Yanga sc Kuwakosa Aucho,Mzize

Yanga sc Kuwakosa Aucho,Mzize

by Sports Leo
0 comments

Kikosi cha Yanga Sc kitaendelea kuwakosa wachezaji wake Khalid Aucho, Clement Mzize ambao ni majeruhi huku Ibrahim Bacca naye akikosekana kutokana na kutumikia adhabu ya kadi nyekundu.

Msafara wa Yanga sc tayari leo umewasili Ruangwa,Lindi kwa ajili ya mchezo dhidi ya Namungo FC utakaofanyika siku ya Jumamosi, Novemba 30 katika uwanja wa Majaliwa mkoani humo.

Ikiwa imetoka kupoteza kwa mabao 2-0 dhidi ya Al Hilal Fc katika mchezo wa klabu bingwa barani Afrika huku pia ikiwa haijapata ushindi katika michezo yake miwili ya ligi kuu ya Nbc,Yangavsc itahitaji alama tatu ili kurejea kwenye ubora wake.

banner

Aucho na Mzize ni wachezaji muhimu klabuni hapo kutokana na ubora wao ambapo kocha Sead Ramovic anaweza kuwatumia Jonas Mkude na Kennedy Musonda katika nafasi hizo.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited