Home Soka Acheni Uzushi-Zahera

Acheni Uzushi-Zahera

by Sports Leo
0 comments

Kocha wa zamani wa Yanga Mwinyi Zahera amekana tetesi zilizosambazwa kwenye mitandao ya kijamii zinazomuhusisha kurejea Yanga

Zahera aliyeweka makazi yake nchini, amesema hakuwasiliana na kiongozi yeyote wa Yanga kuhusu jambo hilo

Mcongomani huyo amesema walioanzisha uvumi huo wana lengo la kumgombanisha na waajiri wake hao wa zamani

banner

“Sio kweli, sijazungumza na kiongozi yeyote wa Yanga.. wanaandika Yanga wameniita tujadiliane ni waongo hakuna jambo hilo, amesema”

“Wanaoandika uongo huo hawana nia nzuri na mimi pamoja na klabu ya Yanga, nawaambia waache kufanya hivyo”

Tangu mkataba wake uvunjwe mwezi Novemba 2019, Zahera ameendelea kubaki nchini ambapo amebainisha kuwa licha ya kupokea ofa kutoka klabu kadhaa, bado hajafanya maamuzi

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited