Balozi wa Uingereza nchini Tanzania David Concar amezitembelea klabu kongwe za soka nchini za Simba sc na Yanga sc kwa lengo la kuzifahamu zaidi pamoja na kukuza uhusiano katika uga wa michezo na nchi yake.
Katika ziara hizo ambazo zilianza yalipo makao makuu ya klabu ya Simba sc Masaki jijini Dar es salaam Balozi huyo alipokelewa na Mwenyekiti wa Bodi ya klabu hiyo Salim Abdalah ‘Try Again’ pamoja na Afisa Mtendaji mkuu wa klabu hiyo Iman Kajula sambamba na mjumbe wa bodi Asha Baraka ambapo alitembezwa katika baadhi ya idara za klabu hiyo pamoja na kufahamishwa mipango mbalimbali ya klabu ikiwemo mchakato wa mfumo wa mabadiliko ya uongozi wa klabu hiyo.
Pia baada ya hapo Balozi huyo alipelekwa katika viwanja vya mazoezi vya klabu hiyo vya Mo Simba Arena vilivyopo Boko ambapo alipata wasaa wa kuzungumza na wachezaji na benchi la ufundi la klabu hiyo.