Nahodha wa klabu ya Simba sc John Boko Ametwaa tuzo ya mchezaji bora wa mwezi juni akiwashinda Atupele Green wa biashara united na Martin Kiggi wa Aliance School ambao aliingia nao fainali.
Boko ametwaa tuzo hiyo akiwa amefunga mabao saba katika ligi kuu huku akiwa katika kiwango bora toka ligi irejee kutoka katika mapumziko ya janga la Corona huku akiwa ametoka kuisaidia Simba sc kushinda taji la ligi kuu bara kwa mara tatu mfululizo.