Aliyekua kipa namba moja wa Yanga Benno Kakolanya amesaini mkataba wa miaka miwili wa kuitumikia Simba Sc akisaini kama mchezaji huru baada ya mkataba wake na klabu ya Yanga sc kuvunjwa na shirikisho la soka la Tanzania (Tff).
Kakolanya amesaini mkataba huo na kumaliza tetesi za yeye kujiunga na klabu hiyo yenye makao yake makuu Msimbazi Kariakoo jijini Dar es salaam huku ikielezwa wakala wake ambaye anafahamika kwa jina la Haroub akicheza nafasi kubwa kufanikisha dili hilo kwa kuwa yeye ni mpenzi wa Simba sc.
🎯 Usipitwe!
Kuwa wa kwanza kupata habari za moto za michezo nchini Tanzania na duniani kwa ujumla, moja kwa moja kwenye barua pepe yako kutoka SportsLeo Bongo!
- ✅ Matokeo ya mechi
- ✅ Uchambuzi wa kina
- ✅ Habari za ndanii ya timu zako pendwa
✉️ Quality content, no spam. Unsubscribe anytime.
Kakolanya alijiunga na Yanga kutokea Prisons ya Mbeya licha ya kutopata nafasi ya kutosha klabuni hapo mbele ya Ally Mustapha na Deo Munishi ambao baadaye waliondoka jangwani na kumuachia ufalme kipa huyo kabla kukorofishana na kocha Mwinyi Zahera aliyegoma kufanya nae kazi.