Home Soka Breaking News..Kakolanya Asaini Simba

Breaking News..Kakolanya Asaini Simba

by Dennis Msotwa
0 comments

Aliyekua kipa namba moja wa Yanga Benno Kakolanya amesaini mkataba wa miaka miwili wa kuitumikia Simba Sc akisaini kama mchezaji huru baada ya mkataba wake na klabu ya Yanga sc kuvunjwa na shirikisho la soka la Tanzania (Tff).

Kakolanya amesaini mkataba huo na kumaliza tetesi za yeye kujiunga na klabu hiyo yenye makao yake makuu Msimbazi Kariakoo jijini Dar es salaam huku ikielezwa wakala wake ambaye anafahamika kwa jina la Haroub akicheza nafasi kubwa kufanikisha dili hilo kwa kuwa yeye ni mpenzi wa Simba sc.

banner

Kakolanya alijiunga na Yanga kutokea Prisons ya Mbeya licha ya kutopata nafasi ya kutosha klabuni hapo mbele ya Ally Mustapha na Deo Munishi ambao baadaye waliondoka jangwani na kumuachia ufalme kipa huyo kabla kukorofishana na kocha Mwinyi Zahera aliyegoma kufanya nae kazi.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited