Home Soka Dante Aigomea Yanga

Dante Aigomea Yanga

by Sports Leo
0 comments

Beki wa klabu ya Yanga Andrew Vicent “Dante” ameiwekea ngumu klabu hiyo kumlipa fedha zake kwa awamu kama inavyofanya kwa mastaa wengine huku akihitaji kulipwa zote kwa mkupuo mmoja.

Staa huyo anaidai timu hiyo kiasi cha shilingi milioni 40 ikiwa ni fedha za usajili pamoja na mishahara ameombwa na klabu hiyo kukubali kulipwa kwa awamu tatu ambapo awamu mbili atalipwa milioni 15 na awamu ya mwisho atalipwa milioni 10.

Kwa mujibu wa Afisa Habari wa klabu hiyo Michael Bumbuli  staa huyo amegoma akihitaji kulipwa fedha zote kwa mkupua mmoja tofauti na ilivyokua kwa mastaa wengine akiwemo Juma Abdul ambaye amejiunga na timu hiyo baada ya kukubali kulipwa kidogo kidogo.

banner

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited