Home Soka Liverpool,Madrid zashinda,PSG yavutwa shati UEFA

Liverpool,Madrid zashinda,PSG yavutwa shati UEFA

by Sports Leo
0 comments

Michuano ya klabu bingwa Ulaya iliendelea tena usiku wa kuamkia leo ambapo Liverpool,Real Madrid na Man City ziliondoka na pointi tau muhimu katika michezo ya kwanza ya makundi.

Liverpool waliakuwa nyumbani iliwabidi kutoka nyuma na kupata ushindi wa magoli 3-2 dhidi ya AC Milan,magoli ya Liverpool yalifungwa na Tomori aliyejifunga(dkk 9),Salah(dkk 49) na Henderson(dkk 69) hku yale ya AC Milan yakifunga na Rebic(dkk 42) na Diaz(dkk 44).

Real Madrid wakiwa ugenini Italia walipata ushindi wa 1-0 dhidi ya Inter Milan lililofungwa Rodrygo dakika ya 89,huku mabingwa wa EPL Manchester City wakiitandika RB Leipzig 6-3 katika mchezo uliojaa mvua ya magoli.

banner

PSG licha ya kuwaanzisha mastaa wake Mbappe,Neymar na Messi kwa mara ya kwanza wameshindwa kupata ushidi baada ya kulazimishwa sare ya 1-1 na Club Bruge ya Ubelgiji.

Matokeo mengine;

Atletico Madrid 0-0 FC Porto

Sporting 1-5 Ajax

Sheriff 2-0 Shakhtar Donetsk

Besiktas 1-2 Dortmund.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited