Home Soka Maradona Hoi,Kisa Pombe

Maradona Hoi,Kisa Pombe

by Sports Leo
0 comments

Mchezaji mkongwe Diego Maradona ametolewa hospitali siku ya Jumatano, na kuelekea kliniki ya kurekebisha tabia ili kuacha kutegemea pombe. Maradona, aliliongoza taifa lake katika mashindano ya kombe la dunia ya mwaka 1986,. Alifanikiwa kufanya upasuaji katika ubongo ili kuondoa kuganda kwa damu, mapema mwezi huu.

Hata hivyo , tatizo la utegemezi wa pombe limemfanya akae hospitalini kwa muda mrefu. “Jambo zuri ni kuwa Diego yuko sawa sasa,” alisema wakili wake, Matias Morla. Wiki iliyopita, Maradona alilazwa katika kliniki ya Ipensa huko Buenos Aires , akiwa anasumbuliwa na anaemia .

Rafiki zake wachache tu ndio waliruhusiwa kumtembelea hospitalini. Wakili wake amesema Diego amepitia kipindi kigumu zaidi katika maisha yake na ilikuwa kama miujiza kukuta damu imeganda katika ubongo wake na angeweza hata kupoteza maisha yake.

banner

Cc:Sammisago

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited