Home Soka Mbeya City Yamfungua Mdomo Nahodha Yanga

Mbeya City Yamfungua Mdomo Nahodha Yanga

by Sports Leo
0 comments

Nahodha Msaidizi wa Yanga Juma Abdul amesema matokeo ya sare ya bao 1-1 dhidi ya Mbea City hawakuyatarajia, lakini ndivyo mpira ulivyo.

Katika mchezo huo ambao Yanga ilitawala kila idara, ilitengeneza nafasi nyingi lakini waliweza kutumia nafasi moja tu.

“Dah! sijui hata niseme nini ila acha tumuachie yeye mwenyewe muumba sababu alishapanga iwe vile”

banner

“Hapo ndipo utakapojua mchezo wa mpira una matokeo ya kikatili.. lakini tunakushukuru mungu wetu hata kwa hiki kidogo ulichotupatia inshaallah,” ameandika Abdul kwenye ukurasa wake wa mtandao wa Instagram

Kwenye mchezo huo bao la Yanga lilifungwa na Bernard Morrison lakini likipita mguuni kwa Abdul ambaye msimu huu amerejea kwenye makali yake

Abdul amehusika kwenye mabao matano ya Yanga mpaka sasa msimu huu katika michezo ya ligi kuu

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited