Home Soka Misri Waanza Vizuri Afcon

Misri Waanza Vizuri Afcon

by Sports Leo
0 comments

Timu ya Taifa ya Misri imeanza vizuri michuano ya mataifa ya Afrika baada ya kuibuka na ushindi mwembamba wa bao moja kwa bila dhidi ya Zimbabwe katika mchezo wa ufunguzi wa michuano ya hiyo uliochezwa jana usiku.

Wenyeji wakiongozwa na mshambualiaji hatari anayeichezea Liverpool ya Uingereza Mohamed Salah walianza mchezo kwa mashambulizi ya mara kwa mara langoni mwa zimbabwe japo walikosa nafasi kadhaa za kufunga magoli.

Iliwalazimu wenyeji kusubiri mpaka dakika ya 41 kipindi cha kwanza kupata bao lililiwekwa kimiani na mshambualiaji Mahmoud Trezeguet anayeichezea klabu ya Kasimpasa ya nchini Uturuki.

banner

Hata hivyo kinyume na matarajio ya wengi mshambualiaji Mohamed Salah alishindwa kufumania nyavu katika mchezo huo huku kwa upande wa Zimbabwe Kalma Billiat akifanikiwa kuwasumbua wenyeji.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited