Home Soka Molinga Aikoa Yanga sc

Molinga Aikoa Yanga sc

by Sports Leo
0 comments

Straika wa klabu ya Yanga David Molinga ameibuka shujaa katika mchezo dhidi ya Namungo Fc baada ya kusawazisha mabao mawili na kuifanya mechi kumalizika kwa sare ya 2-2 katika mchezo wa ligi kuu uwanja wa Taifa.

Awali Namungo walitangulia kupitia mabao ya Charles Edward aliyofunga dakika za 51 na 69 lakini kuingia kwa David Molinga kipindi cha pili kulibadili hali ya hewa baada ya kufunga mabao ya kusawazisha dakika za 79 na 95 na kufanya mchezo kumalizika kwa sare.

Yanga wamesalia nafasi ya tatu huku Namungo wakibaki nafasi ya nne ambapo Simba anaongoza ligi kwa jumla ya pointi 81 huku Azam fc ambaye alipoteza mbele ya Kagera Sugar akibaki nafasi ya pili.

banner

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited