Sintofahamu imeibuka katika klabu ya Yanga sc baada ya staa wa timu hiyo Benard Morrisson kutosafiri na timu huku ripoti zikidai kwamba staa huyo amezima simu.
Taarifa za ndani zinadai kwamba staa huyo hafurahishwi na jinsi mambo yanavyoendeshwa klabuni humo ikiwemo suala la timu kusafiri umbali mrefu kwa basi kuelekea mkoani Shinyanga.
Hata hivyo baadhi ya taarifa zinasambaa kuwa mkataba wa staa huyo unaisha wiki ijayo na anataka asainishwe mpya kama walivyokubaliana kwa kiasi cha dola elfu sabini ambazo anataka alipwe kwa wakati mmoja.
🎯 Usipitwe!
Kuwa wa kwanza kupata habari za moto za michezo nchini Tanzania na duniani kwa ujumla, moja kwa moja kwenye barua pepe yako kutoka SportsLeo Bongo!
- ✅ Matokeo ya mechi
- ✅ Uchambuzi wa kina
- ✅ Habari za ndanii ya timu zako pendwa
✉️ Quality content, no spam. Unsubscribe anytime.