Home Soka Msuva Aikoa Stars

Msuva Aikoa Stars

by Sports Leo
0 comments

Winga wa Diffaa El-Jadid ya Morroco Saimon Msuva ameisaidia Tanzania kupata sare  ya bao 1-1 dhidi ya Burundi baada ya kusawazisha goli la Cedrick Amis lililofungwa dakika ya 81.

Msuva aliipatia Stars bao hilo dakika ya 86 baada ya mabeki wa timu hiyo kujichanganya kufuatia shambulizi la kushtukiza lililofanywa na Taifa stars.

Licha ya sare hio stars ilijitahidi kukwepa hujuma baada ya kuhisi kupuliziwa dawa vyumbani hali iliyowasababisha wachezaji kwenda mapumziko kwenye mabenchi ya uwanjani badala ya vyumbani.

banner

Mechi hiyo ya kuwania kufuzu fainali za kombe la dunia nchini qatar mwaka 2022 itarudiwa siku ya jumamosi septemba 8 nchini katika uwanja wa taifa jijini Dar es salaam.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited