Home Soka Nonga,Lipuli Watibuana

Nonga,Lipuli Watibuana

by Sports Leo
0 comments

Nahodha wa klabu ya Lipuli Fc Paul Nonga hajajiunga na kambi ya timu hiyo kufuatia kutomaliziwa malipo yake hasa mshahara na dau la usajili la mkataba wa sasa.

Straika huyo aliyecheza timu kadhaa nchini Ikiwemo Yanga sc,Mbeya city na Mwadui Fc alisaini mkataba wa mwaka mmoja na Lipuli Fc ambao unaisha mwishoni mwa msimu huu.

“Ni kweli sijaripoti kambini lakini sijagoma ila kuna mambo ya kimkataba ambayo hayaja timizwa. Sijalipwa mshahara wa miezi mitatu pia dau langu la usajili sijamaliziwa na niliuambia uongozi wanalipe hata nusu lakini mpaka sasa naona ni kimya,”  Alisema Paul Nonga, Nahodha wa Lipuli FC.

banner

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited