Home Soka Ole aondoka rasmi Old Trafford

Ole aondoka rasmi Old Trafford

by Sports Leo
0 comments

Klabu ya soka ya Manchester United imethibitisha kuachana na kocha wake mkuu Ole Gunnar Solskjaer mchana huu kupitia taarifa rasmi ya klabu iliyotolewa kwenye mitandao rasmi ya timu hiyo.

Man Utd na Ole wamekubaliana kusitisha mkataba wa kocha huyo uliokuwa ukimalizika mwaka 2025 kwa heshima,huku ikimtaja na kumshukuru kwa mchango mkubwa wa kuijenga timu hiyo.

Michael Carrick ametangazwa kuwa kocha wa muda wakati ambao klabu inatafuta kocha wa mpito hadi mwisho mwa msimu huu,kabla ya kutangaza rasmi kocha mpya msimu utakapoisha.

banner

Carrick ameomba kuendelea kusalia kwa Mike Phelan na Kieran McKenna kama sehemu ya benchi la ufundi kuelekea mchezo wa ligi ya mabingwa Ulaya dhidi ya Villareal siku ya Jumanne na ule dhidi ya Chelsea wikiendi ijayo.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited